Recent Posts

Wednesday, October 17, 2012

HONGERENI WAZANZIBARI marufuku ya Pombe,Sigara Na Ukahaba Zanzibar

Posted by Unknown 1:53:00 AM, under | No comments


Serikali ya Mapinduzi Zanzibar imepiga marufuku biashara ya ukahaba, matangazo yote ya pombe na uvutaji wa sigara katika mikusanyiko ya watu katika visiwa vya Unguja. Hayo yamebainika kufuatia marekebisho ya kifungu cha sheria cha 112, cha mswada wa sheria kuhusiana na hifadhi na usimamizi wa vihatarishi vya afya ya jamii na afya ya mazingira na mambo yanayohusiana na hayo iliyopitishwa ndani ya Baraza la Wawakilishi jana.Waziri wa Afya Zanzibar Juma Duni Haji aliwaambia wajumbe wa Baraza la Wawakilishi kwamba kutokana na michango mingi ya wajumbe kutaka suala la matangazo ya pombe, uvutaji wa sigara, na biashara ya ukahaba vipigwe marufuku, serikali imekubaliana na maoni ya wajumbe hao. Waziri Duni amesema, kuanzia sasa kwa mujibu wa sheria hiyo itakuwa ni marufuku kutangaza au kushajiisha matangazo ya pombe kwa kutumia njia mbalimbali zikiwemo ufadhili au matamasha ya muziki na starehe katika visiwa hivyo. Mwanasheria Mkuu wa Zanzibar, Othman Masoud Othman alisema anakubaliana na maoni ya wajumbe wa Baraza la Wawakilishi kuondoa kabisa matangazo ya pombe na kwamba serikali imefanya vyema, kwani hivi sasa Shirika la Afya Duniani WHO, Umoja wa Ulaya EU na baadhi ya nchi ikiwemo Sweden tayari zimezuia matangazo ya pombe na Zanzibar kufuata sheria hiyo ni jambo la busara.

WAKUTANAPO WAKUU WA NCHI>>>>>>SULTANI QABOOS WA OMAN AMTUNUKU NISHANI YA HESHIMA RAIS JAKAYA KIKWETE

Posted by Unknown 1:23:00 AM, under | No comments


Sultani wa Oman,Qaboos bin Said Al Said (kulia)  akimtunuku Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete wa Tanzania, Nishani ya juu ya heshima ya Taifa la Oman wakati wa dhifa ya kitaifa iliyoandaliwa kwa heshima ya Rais Kikwete na ujumbe wake jana jioni katika kasri ya  AL Alam jijini Muscat Oman.
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akimkabidhi zawadi mwenyeji wake Sultani wa Oman Qaboos bin Said Al Said katika kasri ya AL Alam jijini Muscat Oman jana jioni muda mfupi kabla ya dhifa ya kitaifa aliyoandaliwa kwa heshima yake.
Sultan Qaboos bin Said Al Said akimpongeza Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete baada ya kumtunuku nishani ya juu ya heshima ya Taifa la Oman jana jioni katika kasri ya AL Alam, Jijini Muscat Oman jana jioni .Rais Kikwete aliwasili nchini Oman jana jioni kwa ziara rasmi ya siku tatu.
Picha na Freddy Maro.HABARI KWA MSAADA WA aloyson.blogspot.com

BREAKING NEWS: HATARIIIIIIIIIIIII............... Bweni lanusurika kuteketea katika chuo cha UTUMISHI WA UMMA (TPSC) TABORA

Posted by Unknown 1:10:00 AM, under | No comments


 Hiki ndicho chumba moto ulipoanzia
Bweni hilo la wasichana maarufu kwa jina la Shaaban Roberth limenusurika kuteketea kwa moto usiku huu kwa kuanza kuungua moja ya chumba kilichopo flow ya juu katika bweni hilo, ikiwa dalili za awali zinaonesha chazo ni shoti ya umeme kwenye switch ya ukutani (Wall Switch Socket).
Juhudi za kuokoa zilifanikiwa mapema na kuzuia moto huo kuendelea kuteketeza bweni hilo, zana za fire extinguisher zilitumika na hatimaye kuokoa athari ambazo zingetokea. Hata hivyo kikosi cha zimamoto hakikuchelewa kufika eneo la tukio.
Pia mmoja kati ya wanachumba hicho alizimia baada ya tukio hilo kutokea.
HABARI: KWA MSAADA WA ALOYSON.BLOGSPOT.COM

Friday, October 5, 2012

MARIO BALOTELLI ARUDIANA NA MPENZI WAKE WA ZAMANI

Posted by Unknown 12:17:00 AM, under | No comments


Mchezaji wa Manchester City Mario Balotelli akiwa na mpenzi wake Raffaella mwenye ujauzito, waliachana April 2012 baada ya kuwa kwenye uhusiano wa kimapenzi kwa mwaka mmoja, sasa hivi wamerudiana tena.
.
.

SABABU ZA TIMU YA YANGA KUMTIMUA KOCHA TOM SAINTFIET

Posted by Unknown 12:06:00 AM, under | No comments

  

Wote wametimuliwa Yanga
Fukuza fukuza ya klabu ya Yanga iliyoanza leo mchana baada ya mkutano wa wajumbe wa kamati ya utendaji uliofanyika leo katika makao makuu ya klabu imeendelea imemkumbuka kocha mkuu wa klabu hiyo Mbelgiji Tom Saintfiet.

Taarifa za uhakika kutoka kwa makamu mwenyekiti wa klabu hiyo Clement Sanga ni kwamba  uongozi wa timu hiyo umefikia maamuzi ya kumtimua kazi kocha huyo aliyeajiriwa miezi mitatu iliyopita kutokana na kutofautiana sera za namna ya kuiendesha klabu na uongozi wa juu wa mabingwa hao wa Afrika mashariki na kati.

Mchana leo kamati ya utendaji ilisimamisha ajira za viongozi waajiriwa wote wa klabu hiyo akiwemo katibu mkuu Celestine Mwesigwa na msemaji Luis Sendeu huku ikitoa onyo kwa kocha Saintfiet kwa tabia yake ya kuongea na waandishi wa habari bila mpangilio wa klabu. Lakini baada ya taarifa hizo kutoka usiku wa leo kocha huyo akaonekana akiongea kwenye television mojawapo nchini akizungumzia mambo mbalimbali kuihusu Yanga.

Kwa mujibu wa Sanga anasema kwamba sakata lote la jinsi kocha huyo alivyopoteza kazi yake litatolewa ufafanuzi hapo kesho.

Wakati huo huo aliyekuwa katibu mkuu wa Yanga kabla ya Mwesigwa, Lawrence Mwalusako amepewa jukumu la kukaimu nafasi hiyo ya ukatibu mkuu wa Yanga kwa muda, wakati mchezaji wa zamani wa klabu hiyo Seikolojo Chambua amekabidhiwa majukumu ya kuwa meneja wa timu hiyo akichukua nafasi ya Hafidh Salehe ambaye nae aliondolewa leo mchana.

Nafasi ya usemaji wa Yanga mpaka sasa imekuwa kitendawili, tetesi zinasema kuwa mtangazaji wa Clouds FM NA Clouds TV Abdul Mohamed na Mwanahabari Mahmoud Zubeiry mmojawapo anaweza kula shavu la kumrithi Sendeu.

Thursday, October 4, 2012

ZITTO KABWE KUGOMBEA URAISI 2015 KWA TIKETI YA CHADEMA.

Posted by Unknown 11:40:00 PM, under | No comments


Mbune wa Kigoma  mh. ZITTO KABWE athibitisha kwamba atagombea URAIS 2015,   hayo ameyasema wakati akihojiwa na mwendesha kipindi cha amplifire Millard Ayo. Zitto kupitia amplifer ya CLOUDS FM akasema ya kwamba Atagombea kupitia CHADEMA kwa hivyo wale mlio na wasiwasi huo ndio ukweli.
Asema kuna watu wanajidai wao ni CHADEMA zaidi ya wengine wakati yeye amekuwa mwanachama wa CHADEMA tokea ana miaka 16......
Miaka 10 ya ubunge inamtosha hivyo anataka kwenda hatua nyingine kisiasa na anazo AGENDA za msingi za kusimamia hivyo yeye ni tofauti na wanasiasa wengine wanaoutaka urais kama sifa 
 
source; CLOUDS FM ANPLIFER NA MILLAD AYO

COMRADE SAMABALA AGOMBEA UENYEKITI WA UVCCM MKOA WA DODOMA

Posted by Unknown 11:34:00 PM, under | No comments


       Mwanasiasa na mwanzilishi wa group maarufu la Tanuru la Fikra katika mtandao maarufu wa facebook, hatimaye amefunguka na sera ambazo zitamwingiza kwenye cheo hicho chipya endapo kama wanachama wa Dodoma (UV-CCM) watamchagua katika kinyang'anyiro hicho. na haya ndio maneno yake kwenye ukurasa wa facebook

‎>----SAFARI NDEFU YA MAFANIKIO INAENDELEA-------->

*...SHUKRANI ZANGU KWA WOTE NINAOWAPENDA...*

Ndugu zangu wana TANURU LA FIKRA Na Watanzania wenzangu wote kwa Ujumla.

Jioni ya Leo napenda kuchukua fursa hii kusema Machache kwenu.:-

1. Kwanza Nachukua fursa hii kumshukuru Mwenyezi Mungu aliyeniumba mimi na akaumba na vyote vilivyomo na mwenye Kumiliki kila kitu. Mfalme wa Wafalme.

2. Pili Napenda kuwashukuru zaidi Wazazi wangu wawili kwa Kunileta duniani, kunilea kimaadili KIIMANI na Kimazingira. Hayo yote ndio yamenifikisha hapa nilipo na kufahamiana na kila Mmoja.

3. Tatu napenda kuwashukuru zaidi walimu wangu toka ngazi ya awali mpaka Chuo kikuu kwa kunifundisha na kunilea kutaaluma.

4. Na nne napenda kuishukuru Kamati Kuu ya CCM (CC) na NEC Kwa busara walizotumia na hatmaye kuniteua kuwa Mgombea wa Mwenyekiti wa VIJANA DODOMA, Na NEC kupitia wilaya ya Chemba.

Kwa kweli wamenipa Heshima kubwa sana kama Kijana na Mtoto wa Masikini wa Kijijini nisiye wa Ukoo wa 'KIFALME' sitokani na Tabaka la Viongozi. Naahidi Kufanya Makubwa...

Nami Kama Sambala mtoto wa Mzee Unda wa Kijiji cha Mondo Naahidi kuilinda heshima hiyo kwa Kufanya Kampeni Kistarabu, na pia ntakapopata Ushindi basi Ntawatumikia walionipa Nafasi.

Mwisho Niwaombe wote muendelee Kuniombea na Kuniunga mkono kwa Hali na Mali ili kufanikisha ushindi wangu.

NAWAAHIDI VIJANA WENZANGU WA KITANZANIA NA DODOMA NA KONDOA/CHEMBA KUWA SITAAWANGUSHA.

NA PIA NAWAAHIDI NTAKITUMIKIA CHAMA NA UMMA NA SITAMTUMIKIA MTU KWA MATAKWA YAKE.

KWA PAMOJA TUTASHINDA..

''...ONE VOICE MANY VOTES FOR SAMBALA....''

VIJANA NGUVU YA CHAMA..

Tags

Total Pageviews

Labels

Blog Archive

Translate