Recent Posts

Wednesday, July 4, 2012

TEACHING PRACTICE / NYANJANI KWEMA.

Posted by Unknown 10:47:00 PM, under | No comments

Nawatakia mazoezi mema ya mafunzo kwa vitendo huko mwendako ila tujichunge tabia kila mtu awe mlinzi wa mwenzake usikubali mtu hata mmoja akushushie heshima udharaulike/mdharauliwe kisa anatafuta umaarufu. Usikubali kuipoteza nafasi adimu ya masomo uliyoipata pengine kwa kusubiri miaka kadha au kwa matokeo ya kubangaiza.
      Jiepusheni na vile vinavyoitwa teaching practice allowance mwalimu ni kioo cha jamii, jiheshimu utaheshimiwa ukijidharau utadharauliwa MWENYEZI MUNGU awe nanyi nyote muwapo mazoezini.

MWAKA WA MASOMO HUOOOOOOOOO UMEKWISHAAAAAAAAAAAAAAAAAAAA

Posted by Unknown 10:35:00 PM, under | No comments

        Hongereni wanafunzi wote wa Chuo Kikuu Kishiriki cha Kumbukumbu ya Askofu Mkuu Mihayo-Tabora (AMUCTA) kwa kumaliza vyema mitihani ya mwisho ya semista ya pili kwa wanachuo wa mwaka wa kwanza na wa Pili. Tumuombe Mwenyezi Mungu atuwezeshe kuanza vyema mwaka mpya wa masomo kwa mwaka wa 2012/13 na kuumaliza salama salmini.
      

Sunday, June 10, 2012

SHERIA MPYA ZA MAVAZI KWA WANACHUO WA AMUCTA(SAUT-TABORA)

Posted by Unknown 8:24:00 PM, under | No comments

Katika hali isiyotarajiwa na wanafunzi wengi,yaani sawa na kumchekesha aliyenuna, Mwadili( DEAN OF STUDENTS) wa CHUO KIKUU KISHIRIKI CHA KUMBUKUMBU YA ASKOFU MKUU MIHAYO TABORA(AMUCTA) ametoa tangazo la taratibu za mavazi kwa wanachuo wote yaani wake kwa waume. Kuanzia tarehe 18/06/2012 ambayo ni siku ya kuanza mitihani ya kumaliza semista ya II kwa mwaka wa masomo wa 2011/2012 kwa wanachuo hakuna ruhusa ya kuvaa jezi, kaptula/bukta nguo zozote za michezo isipokuwa kwa matukio husika T-shirt round collar, jeans, vimini, vibode tait, kata vitovu, sosk chupi,suruali kwa wanawake, blauz kata mikono zenye kuacha sehemu za mwili wazi nk. Uamuzi huo umefikiwa wakati uvaaji jezi kwa  wanachuo umekuwa kama sehemu ya sare za chuo hiko mfano utakuta jez za aina mbalimbali za chelsea, man u man city liverpool nk. Hii imeamuliwa kulinda maadili kwa wanafunzi wote na kuheshimu na kutunza maadili ya kanisa katoliki la kutosapoti mambo ya anasa ambayo ni kinyume na utamaduni wetu na kumuheshimu MUNGU.
 Kwa ufafanuzi wa nini adhabu zake kwa atakayekiuka utatolewa na Mwadili huyo tarehe 13/06/2012 moja ya kumbi za chuoni hapo.EWE MWANAAMUCTA USIKOSE SIKU HIYO UJUE NINI KITAZUNGUMZIWA ISILE KWAKO.

Friday, April 13, 2012

TAARIFA YA WAZI KWA WANAAMUCTA

Posted by Unknown 3:45:00 AM, under | No comments

Test ya kifaransa imeahirishwa mpaka wiki ijayo kati ya Alhamisi ,Ijumaa au Jumamosi. Taarifa hii ni kwa mujibu wa Rais wa AMUCTASO kama ilivyotolewa na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje kwa niaba ya Rais na serikali ya AMUCTASO kwa ujumla.UKIISOMA MWAMBIE NA MWENZIO.

Tags

Total Pageviews

Labels

Blog Archive

Translate