Recent Posts

Sunday, January 6, 2013

PIGO JINGINE KWA TASNIA YA SANAA ZA MAIGIZO NA FILAMU NCHINI TANZANIA.

Posted by Unknown 11:05:00 PM, under | No comments

Msanii wa tasnia ya sanaa ya maigizo na filamu SAJUKI (JUMA KILOWOKO) alifariki dunia jana tarehe 02 Januari,2013 katika hospitali ya taifa ya Muhimbili. Msanii huyo amefariki kwa upungufu wa damu baada ya kuugua muda mrefu. Kabla ya kifo chake marehemu alishakwenda nchini India kupata matibabu ya maradhi yanayomsumbua kupitia michango mbalimbali iliyochangwa na watanzania waliokuwa na mapenzi mema naye kupitia kampeni maalumu iliyofanywa na watu mbalimbali akiwemo mchekeshaji gwiji nchini Massanja Mkandamizaji wa Orijino Komedi nchini Tanzania. marehemu ameacha mke mmoja Wastara ambaye alikuwa anaigiza naye katika filamu na mtoto mmoja. Sajuki atakumbukwa kwa kazi zake nyingi za sanaa tangu akiwa kundi la Kaole Sanaa Group la jijini Dar es Salaam nchini Tanzania.Katika fani ya filamu, marehemu ameigiza filamu kadha wa kadha kama vile MBONI YANGU, MCHANGA NA KENI pamoja na HERO OF THE CHURCH(SHUJAA WA KANISA) aliyoigiza na marehemu Steven Kanumba na nyinginezo nyingi. Naibu Waziri wa Nishati na Madini Mh. January Makamba jana akihojiwa na kituo cha redio cha Clouds FM, alisema alimfahamu marehemu SAJUKI kama kijana aliyekuwa na malengo ya kufika mbali kisanaa na kimaisha kiujumla. Sajuki alikuwa na mpango wa kuandaa tamasha kubwa la kuwashukuru Watanzania wote waliomchangia michango mbalimbali ikiwemo fedha na sala zao kipindi chote alichokuwa anaumwa akiwa nchini na baada ya kwenda nchini India kupata matibabu ya maradhi yanayomsibu. Baba wa marehemu Mzee Kilowoko akihojiwa na vyombo vya habari alisema mwili wa marehemu utazikwa jijini Dar siku ya Ijumaa badala ya Songea mkoani Ruvuma kwenye asili ya babu zake ili kuruhusu watanzania wengi kushiriki mazishi ya Sajuki. Kifo hiki kimetokea ghala muda mfupi tu baada ya kuusheherekea mwaka mpya wa 2013, ikiwa ni siku chache kabla ya watanzania kusahau machungu ya kuondokewa na msanii mwingine wa filamu Shoro Millionea aliyefariki mwishoni mwa mwaka 2012 na kumbukumbu mbaya kabisa ya kuondokewa na nyota nyingine ya filamu Afrika marehemu Steven Kanumba Kazi yake Mola haina makosa mwenzetu ametutoka hatuna budi kumuombea alazwe mahala pema peponi AMINI.

MSUGUANO NDANI YA CHADEMA WANACHAMA WAANZA KUFUKUZANA NA KUVUANA UANACHAMA

Posted by Unknown 10:59:00 PM, under , | No comments

TAARIFA HII IMETOKA MOJA KWA MOJA KWENYE MIKONO YA BAADHI YA WAJUMBE WA KIKAO CHA KAMATI TENDAJI YA VIJANA (BAVICHA) Ndugu Wanajukwaa, Taarifa za kuvuliwa uanachama kwa Juliana Shonza (Makamu Mwenyekiti BAVICHA), Mtela Mwampamba na Habib Mchange ni za kweli! Hatua hii ilifikiwa jana na kikao cha kamati tendaji ya BAVICHA iliyokutana pale Ukumbi wa Mbezi Garden majira ya Saa sita na nusu Mchana. Kikao hiki kimsingi hakikuweka wazi ajenda za kwenda kujadili uanchama wa wahusika hapo juu (Pitia taarifa ya Tumaini Makene hapa JF kuhusu kikao hicho) licha ya wahusika hao hapo juu kualikwa kuhudhuria kikao hicho. Wajumbe walioalikwa kwa ajili ya kikao hiki ni kama wafuatao: (Hawa wahusika si wajumbe wa kikao cha kamati tendaji BAVICHA) 1. Ben Saanane 2. Chacha Hatari 3. Habib Mchange 4. Mtela Mwampamba 5. Gwakisa Burton Mwakasendo. Hao wajumbe hapo juu walihojiwa na kamati tendaji kila mmoja kwa nafasi yake na mashitaka yake mbele ya Mwenyekiti wa Baraza la vijana Ndugu John Heche na katibu Deo Munishi. Naomba kuyaweka mahojiano kama ifuatavyo, (mahojiano yalianza kufanyika saa tatu na nusu usiku). Ben sanaane alihojiwa kwanini ametoa shutuma kali mitandaoni kwa viongozi wake wa juu (Zitto)? Majibu ya msingi ya Ben Saanane yalikuwa ni kwamba aliamua kufanya vile kwasabu ya kukilinda chama na viongozi wake wasihafuliwe mitandaoni na vijana aliowataja ni 'Masalia'. Swali likaja; yeye haoni kama alikuwa anamchafua Zitto ambaye ni kiongozi wa chama? Jibu lake lilikuwa ni kuomba radhi amekosea. Mtela mwampamba alihojiwa kwa kuulizwa mashitaka mawili. Moja ni kwanini anampinga Dr. Slaa kuwa anamiliki kadi ya CCM na pili kwanini alimkashifu Dr. Slaa hapa JF kwa kutumia 'Verified Account'Majibu ya Mwampamba ni kama ifuatavyo:Kwanza alianza kwa kuomba kubadilishiwa mwenyekiti wa kikao kwasababu hana imani naye. Kwanini hana imani naye? Ni kwa sababu wana 'conflict of interest' kwenye siasa (kuanzia kwenye uchaguzi wa BAVICHA) hawaelewani hivyo anaamini haki haitatendeka endapo Heche atasimamia mahojiano yale. Mjumbe mmoja (mwenyekiti Arusha) akanyoosha mkono kwa kusema asiwasumbue wapo kazini. Mwampamba akajibu, hata mbunge wa Arusha Godbles Lema aliomba kubadilishiwa jaji kwenye kesi yake kwasababu alikuwa hana imani naye. Mwampamba akaongeza kwa kusema Ibara ya 18 na 19 ya katiba mama ya nchi inampa uhuru wa kuchagua nani wakusikiliza maoni yake na haki ikatendeka. Mjumbe mwingineakasimama akasema kuwa yeye ameacha kata yake na kuja kusikiliza, Mwampamba unatusumbua. Mwampamba akamjibu mimi nimeacha wanachi 32,000 kule Mbozi jimboni (alikogombea ubunge mwaka 2010) wanaonitegemea nimekuja hapa, wewe unataka kusema ndio unajua sana kazi? Kilichotokea: Bwan John Heche akagadhabika na kuamuru mabaunsa sita (6) wakiongozwa na Baunsa wa Mbowe anayejulikana kwa jina la 'Swai' wamtoe nje. Mwampamba alitolewa nje kwa nguvu, akatoka!HABIB MCHANGE:Yeye alikuwa na shitaka la kuwakashifu viongozi mitandaoni. Habib Mchange akahoji kwa mwenyekiti wa kikao. Kwanza alihoji uhalali wa kikao, kwasababu kile kikao kikatiba hakipo kwasababu hakuna makatibu wa baraza la vijana ni kikao cha wenyeviti tu? Pia, akaomba aelezwe ameitwa kama nani kwenye kikao kile? Pia akaomba apewe mashitaka yake yenye uthibitisho wa yeye kuhusika na hayo wanayo yasema. Mwenyekiti kwa hasira akaamuru mabaunsa wamtoe Mchange nje! Mchange kwa ustaarabu akatoka nje.Gwakisa Burton:Yeye alikuwa na mashitaka mawili la kumpinga Dr. Slaa kuwa na kadi mbili ya CHADEMA na CCM pamoja na kumpinga Sugu Mbunge wa Mbeya mjini (CHADEMA). Bila kuchelea Gwakisa akakili kweli alimpinga Dr. Slaa kwa kumiliki kadi mbili, Pia alikili alimpinga Sugu kwasababu wanatofautiana kimawazo (ikumbukwe Gwakisa alitolewa kwenye kura za maoni jimbo la Mbeya Mjini ili Sugu apitishwe kuwa mgombea). Alichokifanya mwenyekiti John Heche palepale akaamuru kumsamehe Gwakisa na kupewa onyo kali la kutorudia tena kuwapinga viongozi wake. Ndugu wana JF, Kikao kilimalizika mnano saa 5 na dakika 46 usiku. Maazimio ya kikao kile ni kuwavua uanachama wahusika watatu hapo juu. UTATA ULIPOJITOKEZA: Kimsingi katiba hairuhusu kabisa na haiwapi mamlaka BAVICHA kufukuza uanachama mtu yeyote. Kwenye katiba hakuna sehemu kamati tendaji inapewa nafasi ya kuhoji na kufukuza wanchama ndani ya chama. Pia, Juliana Shonza atavuliwajwe uongozi na kamati tendaji wakati katiba inaeleza wazi kuwa mkutano mkuu utaitishwa lilikumvua uongozi kwa sababu yeye alichaguliwa na mkutano mkuu? HATUA ALIYOICHUKUA FREEMAN MBOWE: Nimetoka makao makuu ya CHADEMA muda huu pale Kinondoni, wameandaa toka asubuhi eneo, ambapo palitakiwa pafanyike Press Conference na vyombo vya habari kuhusu maazimio ya jana kwenye kikao. Freeman Mbowe amezuia hatua hiyo ya kutangaza maazimio hayo kwa sababu BAVICHA hawana mamlaka ya kumuwajibisha mwanachama yeyote, Kinachotakiwa BAVICHA kukifanya ni kupeleka mapendekezo yao kamati kuu ya CHADEMA taifa ndiko maamuzi yote yatafanyika. Kwa maana hiyo John Heche na Mbowe wapo kwenye msuguano mkali,Kutokana na kwamba hili swala likifika kamati kuu litakwend akinyume na wanavyotaka.wajumbe wengi wa kamati kuu wanaendesha mamuzi yao kiutuuzima,bila hisia na kikatiba. Pia uzito wa makosa haya haupelekei kupoteza vijana hawa wenye umuhimu mkubwa kwenye majimbo yao na kwenye chama.KUHUSU JULIANA SHONZA:Yeye hakufika kwenye kikao kile kutokana na kutokuwepo jijini Dar es Salaam na taarifa kuchelewa kumfikia. Hivyo walishindwa kufanya mahojiano naye na kumpatia mashitaka yake. HALI NDANI YA KIKAO ILIVYOKUWA: Wajumbe walionekana kuandaliwa ipasavyo kisaikolojia kwaajili ya kuwakabili Mwampamba na Mchange. Kwa sababu walipoingizwa kwenye ukumbi wa kikao kila mmoja alitengewa kiti chake na kukabishiwa mabaunsa 6 kwa ulinzi. Muda wote Mwampamba na Mchange walikuwa kwenye ulinzi mkali sana. Waalikwa wengine kama Saanane na Gwakisa na hatari walikwa hawana ulinzi, wapo free. MWISHO: Hii ndio CHADEMA, kuna uwezekano wa wanachama wengi wakafukuzwa kwa kupigiwa simu tu bila katiba kufuatwa. Pia kufukuza wanachama ndio last solution kwa kulea vijana? SOURCE:JAMIIFORUM/Jukwaa la siasa

Tuesday, December 4, 2012

NGASSA ANG'AA MTANDAO WA GOAL.COM KUPITIA TWITTER

Posted by Unknown 9:45:00 PM, under | No comments

World Player of the Week DECEMBER 1-7, 2012 Facundo Ferreyra AGE 21 POSITION Striker FOR Velez Sarsfield WEEK IN NUMBERS APPS (GOALS SCORED) 1 (2) TIME ON PITCH 90 PREVIOUS WINS 0 Velez Sarsfield 2-0 Union de Santa Fe Facundo Ferreyra scored arguably the two most important goals of his fledgling career last weekend, as he struck twice against Union to guide Velez Sarsfield to championship glory in Argentina with a round to spare. The 21-year-old headed home powerfully at the near post to put his side in pole position in the match, before settling matters late on with a superb finish from inside the area to secure a 2-0 win for Velez and leave them with an unassailable five-point lead over Lanus at the top of the Torneo. Not only that, but the two strikes took 'Chucky' Ferreyra's tally to 11 for the tournament, moving him ahead of Newell's Old Boys' Ignacio Scocco in the race for the top-scorer prize. As Pablo Aro Geraldes, chief editor of Goal.com Argentina, says: "He was tournament top scorer, and his goals made it possible for Velez to claim the title, avenging the relegation he suffered with his beloved Banfield. He deserves all the awards." Goal.com International's South America expert Rupert Fryer summed up the striker's whirlwind 12 months: "Ferreyra could have packed his bags for Europe when his club Banfield were relegated last season, but instead decided it might be better for his long-term development to stick around at home a little longer. Having decided to do so, the choice was clear - Boca Juniors or River Plate? Chucky, however, was playing the long game, and so opted for perhaps the most efficiently run club in the country. On Sunday that decision was truly vindicated. Congratulations to Facundo Ferreyra, Goal.com's 185th World Player of the Week winner! The Shortlist Omar Gonzalez - LA Galaxy ‏@Conrad_Osei: "He scored and contributed a huge amount to their win against Houston." Goal.com's Zac Lee Rigg: "Beckham kept sending the ball into the box, and Gonzalez simply dominated." Michu - Swansea City @Sifsta: "Second goal showed how cool and composed he is." Goal.com's Jamie Dunn: "Scored twice in the final few minutes to make sure Swansea got their reward." Mrisho Ngassa - Tanzania @MgayaYahya: "He is simply high-performance." Goal.com's Dennis Mabuka: "He grabbed the headlines, scoring five goals and creating two - scintillating stuff. Cristiano Ronaldo - Real Madrid @dejaiigalactico: "Super goal, great tricks and tracked back when required..inspirational." Goal.com's Luis Herrera: "Madrid were considered underdogs, but Ronaldo responded with gusto."

RAIS BARACK OBAMA WA MAREKANI AMUONYA RAIS WA SYRIA.

Posted by Unknown 9:29:00 PM, under | No comments

AMUONYA DHIDI YA MATUMIZI YA SILAHA ZA KIKEMIKALI DHIDI YA WAPINZANI WAKE RAIS Barack Obama amemwonya rais wa Syria Bashar al-Assad kwamba atawajibishwa endapo majeshi yake yatatumia silaha za kemikali dhidi ya upinzani nchini Syria. Obama alitamka hayo katika kikao hapa Washington kusisitiza msimamo wa Marekani dhidi ya ulimbikizaji wa silaha za nuklia na kemikali wakati wa maadhimisho ya miaka 20 ya mkataba wa ushirikiano wa kupunguza vitisho vya silaha za kemikali kati ya Marekani na Russia. Lakini kilichogonga vichwa vya habari ni onyo lake kwa rais wa Syria, siku moja baada ya Washington kuionya Damascus dhidi ya matumizi ya silaha za kemikali. Obama alisema Marekani itaendelea kuunga mkono azma halali ya raia wa Syria, na kutoa misaada ya kibinadamu kwa upinzani na katika makabidhiano huru ya madaraka pasipo utawala wa Assad. Alimwonya rais Assad kuwa dunia inatizama kinachoendelea nchini Syria na kwamba matumizi ya silaha za kemikali kamwe hayatakubalika. Rais wa Syria, Bashar al-Assad. RAIS WA SYRIA ASSAD. Na ikiwa atafanya kosa la kutumia silaha hizo kutatokea madhara na Assad atawajibika. Obama alisisitiza kuwa dunia haiwezi kuruhusu karne ya 21 kutumbukizwa katika kiza cha karne ya 20 ya matumizi ya silaha kama hizo. Alisema jukumu la kuzuia ugaidi wa kutumia silaha za nuklia ni mojawapo ya maswala yaliyopewa kipaumbele kwa usalama wa kitaifa, na kwamba dunia inasogea mbele kuhakikisha hakuna silaha za nuklia katika siku za usoni.

Thursday, November 29, 2012

COSTRUCTIVISM THEORY

Posted by Unknown 3:06:00 PM, under | No comments

FOR MORE INFORMATION GO TO http://www.learning-theories.com/constructivism.html

Saturday, November 3, 2012

KWA WANAAMUCTA WOTE>>>>>>>>ARCHBISHOP MIHAYO UNIVERSITY COLLEGE OF TABORA ALMANAC - 2012/2013 ACADEMIC YEAR

Posted by Unknown 10:20:00 PM, under | No comments


MONTH
DAY & DATE
ACTIVITY
September
Friday 14th
End of long vacation
Saturday 15th
Arrival and registration of new students
Monday 17th
Supplementary/Special examinations start
Tuesday 18th
Orientation of new students begins
Thursday 20th
Arrival and registration of continuing students
Monday 24th
Convocation Day
Tuesday 25th
Lectures begin
Wednesday 26th
Quality Assurance Committee
Thursday 27th
HODs meeting
Saturday 29th
Academic staff meeting with the Principal
October
Friday 5th
Dean of Students meeting with AMUCTASO
Monday 8th
DPAA meeting with Class Representatives
Tuesday 9th
DPAA meeting with lecturers
Wednesday 17th
Administrative committee meeting
Tuesday 23rd
Academic committee meeting
Thursday 25th
Management Board meeting
November
Thursday 15th
Administrative Committee meeting
Thursday 22nd
Academic Committee meeting
Tuesday 27th
Administrative staff meeting with the Principal
Friday 30th
Management Board meeting
December
Saturday 1st
Quality Assurance seminar
Wednesday 5th
Release of Examination timetable
Thursday 13th
DPAA meeting with Class Representatives
Saturday 15th
AMUCTASO election
Tuesday 18th
Management Board meeting
Saturday 22nd
Christmas break begins
Tuesday 25th
Christmas Day
January
Tuesday 1st
New year day
Friday 4th
End of Christmas break
Saturday 5th
Quality Assurance Committee
Monday 7th
- Lectures resume
- Academic Committee meeting
- Moderation of examinations begins
Tuesday 8th
Finance and Planning Committee
Wednesday 9th
Governing Board meeting
Thursday 10th
AMUCTA Community Day
Saturday 19th
- End of lectures
- Deadline for submission of coursework
Wednesday 23rd
Management Board meeting
Monday 28th
First Semester exams begin
February
Saturday 9th
- End of first semester exams
2
- Short Vacation begins
Thursday 14th
Quality Assurance Committee
Friday 15th
HoDs meeting
Friday 22nd
End of short vacation
Saturday 23rd
Second Semester begins
Monday 25th
Lectures begin
March
Saturday 2nd
Management Board meeting
Wednesday 6th
Examination committee meeting
Friday 8th
International Women’s Day
Monday 11th
Administrative Committee meeting
Monday 18th
Symposium/ seminar/ workshop
Wednesday 20th
Academic staff meeting with the Principal
Wednesday 27th
Easter break begins
Thursday 28th
Good Thursday
Friday 29th
Good Friday
Sunday 31st
Easter Sunday
April
Monday 1st
Easter Monday
Tuesday 2nd
End of Easter break
Wednesday 3rd
Lectures resume
Monday 15th
DPAA meeting with Class Representatives
Tuesday 16th
Academic staff meeting with DPAA
Wednesday 17th
Administrative staff meeting with the Principal
Saturday 20th
Dean of students meeting with AMUCTASO
Tuesday 30th
Management Board meeting
May
Wednesday 1st
Labour Day
Monday 6th
Administrative Committee meeting
Wednesday 8th
HODs meeting
Wednesday 22nd
Management Board meeting
Monday 27th
Moderation of Examinations begins
Friday 31st
Deadline for submission of coursework
June
Tuesday 4th
Quality Assurance Committee
Wednesday 5th
Management Board meeting
Friday 7th
Examination Committee meeting
Friday 14th
End of lectures
Monday 17th
Seminar - Teaching Practice & examinations
Monday 24th
Second Semester Exams begin
Thursday 27th
Distribution of materials for Teaching Practice
July
Saturday 6th
End of second Semester exams
Monday 8th
Supplementary /special exams begin
Monday 15th
Teaching Practice begins
Tuesday 16th
Academic Committee
Wednesday 17th
Finance and Planning Committee
Thursday 18th
Governing Board meeting
3
August
Friday 23rd
End of Teaching Practice
Saturday 24th
Long vacation begins
Tuesday 27th
Examinations Committee meeting
September
Saturday 14th
End of long vacation
Monday 16th
Arrival and registration of new students
Monday 23rd
Supplementary/Special exams start
Saturday 28th
Arrival and registration of continuing students
Monday 30th
Convocation day
October
Tuesday 1st
Lectures begin

Friday, October 26, 2012

NA HAYA NDIYO MANENO YA AFANDE SELE MGOMBEA UBUNGE MTARAJIWA JUU YA NAIBU WAZIRI WA ELIMU BW. PHILIP MULUGO KUHUSU TANZANIA NI MUUNGANO WA KISIWA CHA PEMBA NA ZIMBABWE HUKO AFRIKA KUSINI

Posted by Unknown 9:45:00 PM, under | No comments



Na Millard Ayo
.
Baada ya Naibu waziri wa Elimu na Mafunzo ya ufundi Philipho Mulugo kuomba radhi kwa wote waliomfikiria vingine baada ya kuzungumza kwenye mkutano Afrika Kusini kwamba Tanzania ni muungano wa Pemba na Zimbabwe msanii wa bongofleva Afande Sele ametoa maoni yake.
Sele ambae ameahidi kugombea ubunge wa Morogoro mjini 2015 huku akisisitiza kwamba atakua kwenye chama pinzani na sio CCM namkariri akisema “ni jambo lisilofikirika licha ya dhamana ya uwaziri aliyonayo muheshimiwa Waziri inasikitisha, kitu kibaya ni kwamba yeye ni naibu Waziri wa elimu na hilo swala linahusiana na maswala ya kitaaluma, nchi imepata uhuru mwaka gani, imeingia kwenye muungano mwaka gani, imeungana na nchi gani”
“Inasikitisha kwa sababu ni waziri alafu ni Waziri wa Elimu na swala lenyewe linahusiana na swala la kielimu, kama waziri mwenye dhamana ya elimu anashindwa kutambua basi ndio maana wanasema kwamba mtandao mzima wa serikali yetu basi mara nyingi haufanyi kile ambacho watu wanategemea kwamba kingefanywa vizuri, ndio maana inasainiwa mikataba mibovu kwa sababu mtu anawekwa kwenye  nafasi ambazo hakustahili kuwepo” – Afande Sele
“Hana taaluma, hana uwezo wa kuwa na cheo au mamlaka flani… anapewa kwa sababu ya undugu, urafiki pengine na wale wenye ngazi za juu zaidi ndio wanaochangia kuwa na aina ya mawaziri wa aina ya huyu naibu waziri anashindwa kujua tarehe ya kuungana kwa nchi yetu, kwa hiyo ni mmomonyoko ambao umeanzia juu ambapo ushindi wa yote ni kuivunja nyumba na kujenga upya… swala la kujua tarehe ya uhuru, tarehe ya muungano swala la utaifa kama hilo halihitaji kusema eti mashine iweke sawa au mashine igeuze hata ukikosea maandishi mimi siwezi kukosea kama wewe, hana upeo hana elimu hastahili kuwepo hapo alipo, hata mtoto kama mwanangu Tunda hawezi kukosea jambo kama hilo” – Afande Sele

Tags

Total Pageviews

Labels

Blog Archive

Translate