Recent Posts

Tuesday, January 22, 2013

UGUMU WA MAISHA NA MASLAHI DUNI YASABABISHA ASKARI KUPOTEZA MAISHA KWA AJALI AKISAFIRISHA MIRUNGI

Posted by Unknown 1:57:00 AM, under | No comments

ASKARI wa Kikosi cha Kutuliza Ghasia (FFU) mkoani Arusha PC Samson (20) amefariki dunia akisafirisha mirungi. Kufariki kwa PC Samson kulitokea juzi katika eneo la Mdori mkoani Manyara baada ya kupata ajali ya gari alilokuwa akilitumia kusafirisha mirungi hiyo kutoka Arusha. Taarifa kutoka vyanzo mbalimbali vya habari eneo hilo la Mdori wilayani Babati zilieleza jana kwamba ajali hiyo ilitokea saa 12:30 asubihi.Chanzo cha habari kilichoshuhudia tukio hilo kilisema kuwa gari hilo liliacha njia na kuanguka pembeni mwa barabara,...

ESCAPE FROM SOBIBO ATOROKA GEREZANI NA KUVUA NGUO ASIKAMATWE NA POLISI

Posted by Unknown 1:22:00 AM, under | No comments

Na Nassor Wazambi (facebook) Tabora Manispaa Mwananchi mmoja kwa kushirikiana na askari wa kikosi cha kuzuia ghasia FFU mjini Tabora wamefanikiwa kumkamata mfungwa mmoja wa gereza la mahabusu Tabora wakati akifanya jaribio la kutoroka akiwa amevua nguo na kubakia uchi wa mnyama. Mfungwa huyo ambaye anafahamika kwa jina la Jonas Oscar(25)imedaiwa kuwa mnamo majira ya mchana siku ya tarehe 14 januari 2013 alifanya jaribio...

Friday, January 18, 2013

SERIKALI YATOA SAA 24 KWA UONGOZI WA MAMLAKA YA BANDARI TANZANIA TPA ZIDI YA UBADHIRIFU WA MILIONI 450 FEDHA ZA KITANZANIA

Posted by Unknown 10:12:00 PM, under | No comments

Serikali imetoa masaa 24 kwa Uongozi wa Mamlaka ya Bandari Tanzania TPA kutoa majibu ya uchakachuaji wa mkataba wa Mtambo wa kupakulia mafuta SBM na kusababisha ubadhirifu wa zaidi ya Sh milioni 450. Mkataba huo umedaiwa kubadilishwa kinyemela baada ya kuondolewa kipengele cha mzabuni cha kuendelea kuhudumia vipuri vya mtambo zenye thamani ya kiasi hicho cha fedha kwa kipindi cha miaka miwili. Hayo yamebainika wakati wa ziara ya Mawaziri mbalimbali kwenye Mamlaka ya bandari TPA na hivyo kuzua kitendawili kikubwa kwa mawaziri...

Monday, January 14, 2013

JERRY SILAHA AWASHA MOTO MBEYA AWATAKA UVCCM KUWA MACHO NA WANAOTAKA KUHUJUMU CHAMA KWA MASLAHI YAO

Posted by Unknown 11:42:00 PM, under | No comments

 JERRY SILAA AKIFUNGUA SEMINA YA SIKU MBILI YA VIONGOZI WA UVCCM MKOA WA MBEYA. KUSHOTO  NI AMAN KAJUNA MWENYEKITI WA UVCCM MKOA WA MBEYA KATIBU WA CCM WILAYA YA MBEYA AKIMWAGA SERA ZA CHAMA CHA MAPINDUZI KWA WAKAZI WA NZOVWE MBEYA  AMAN KAJUNA MWENYEKITI WA UVCCM MKOA WA MBEYA AKIMKARIBISHA JERRY SILAA AONGEE NA WANANCHI WA NZOVWE MBEYA JERRY SILAA AKIONGEA NA WANANCHI WA NZOVWE MBEYA VIJANA WA CCM WAKIWA MAKINI...

Sunday, January 6, 2013

P SQUARE UGANDA,WAAPA KUTOKANYAGA TENA NCHI HIYO

Posted by Unknown 11:44:00 PM, under | No comments

Licha ya kupiga show ya nguvu mjini Kampala, Uganda mwezi uliopita, wasanii wa kundi la P-Square wamedaiwa kuapa kutokanyaga tena ardhi ya Uganda kwaajili ya show. Uamuzi huo wameuchukua baada ya kudaiwa kushikiliwa kwa masaa kwenye hoteli ya nyota 5 waliyokuwa wamefikia kwa kushindwa kulipa bili. Waandaji wa show hiyo walikataa kulipa bili hiyo kutokana na kuwa kubwa mno.Kwa mujibu wa vyanzo, mapacha hao Peter na Paul walisaini mkataba na mapromota hao na walilipwa gharama ya kufanyia show huku zile za malazi na usafiri zikiachwa. Hata...

PIGO JINGINE KWA TASNIA YA SANAA ZA MAIGIZO NA FILAMU NCHINI TANZANIA.

Posted by Unknown 11:05:00 PM, under | No comments

Msanii wa tasnia ya sanaa ya maigizo na filamu SAJUKI (JUMA KILOWOKO) alifariki dunia jana tarehe 02 Januari,2013 katika hospitali ya taifa ya Muhimbili. Msanii huyo amefariki kwa upungufu wa damu baada ya kuugua muda mrefu. Kabla ya kifo chake marehemu alishakwenda nchini India kupata matibabu ya maradhi yanayomsumbua kupitia michango mbalimbali iliyochangwa na watanzania waliokuwa na mapenzi mema naye kupitia kampeni maalumu iliyofanywa na watu mbalimbali akiwemo mchekeshaji gwiji nchini Massanja Mkandamizaji wa Orijino Komedi nchini Tanzania....

MSUGUANO NDANI YA CHADEMA WANACHAMA WAANZA KUFUKUZANA NA KUVUANA UANACHAMA

Posted by Unknown 10:59:00 PM, under , | No comments

TAARIFA HII IMETOKA MOJA KWA MOJA KWENYE MIKONO YA BAADHI YA WAJUMBE WA KIKAO CHA KAMATI TENDAJI YA VIJANA (BAVICHA) Ndugu Wanajukwaa, Taarifa za kuvuliwa uanachama kwa Juliana Shonza (Makamu Mwenyekiti BAVICHA), Mtela Mwampamba na Habib Mchange ni za kweli! Hatua hii ilifikiwa jana na kikao cha kamati tendaji ya BAVICHA iliyokutana pale Ukumbi wa Mbezi Garden majira ya Saa sita na nusu Mchana. Kikao hiki kimsingi hakikuweka wazi ajenda za kwenda kujadili uanchama wa wahusika hapo juu (Pitia taarifa ya Tumaini Makene hapa JF kuhusu kikao hicho)...

Pages 81234 »